Atakapotawadha mmoja wenu na akavaa khofu zake (au soksi zake) basi na aswali nazo, na afute juu yake kisha asizivue akitaka kufanya hivyo isipokuwa atakapokuwa na janaba
Choose an available translation of this Hadeeth
Hadeeth text
Imepokewa kutoka kwa Anas -radhi za Allah ziwe juu yake- : Yakwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu -rehema na amani ziwe juu yake amesema: "Atakapotawadha mmoja wenu na akavaa khofu zake (au soksi zake) basi na aswali nazo, na afute juu yake kisha asizivue akitaka kufanya hivyo isipokuwa atakapokuwa na janaba".
Explanation
Benefits
Muda wa kufuta kwa mkazi: Ni mchana na usiku (Masaa 24), na kwa msafiri: Ni michana mitatu na usiku wake (Masaa 72).
Kufuta juu ya Khofu mbili kunahusu tu hadathi ndogo nasi kubwa, ama hadathi kubwa haitakiwi kufuta, bali ni lazima kuvua khofu mbili na kuosha miguu miwili.
Ni sunna kuswali na viatu na khofu na mfano wake na hii ni kwa sababu ya kwenda kinyume na Mayahudi, na hii ni pale viatu vitakapokuwa twahara (visafi), na havina udhia kwa wenye kuswali, au msikiti, mfano kama miskiti iliyotandikwa mabusati mtu hatakiwi kuswali navyo.
Kufuta juu ya khofu mbili kuna urahisi na wepesi kwa umma huu.
Attribution
Categories
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

