Hakika Mwenyezi Mungu aliyetakasika na kutukuka aliteremsha "Na wasiohukumu kwa yale aliyoyateremsha Mwenyezi Mungu basi hao ndio makafiri
Choose an available translation of this Hadeeth
Hadeeth text
Imepokelewa kutoka kwa Bin Abbas -radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- amesema: Hakika Mwenyezi Mungu aliyetakasika na kutukuka aliteremsha "Na wasiohukumu kwa yale aliyoyateremsha Mwenyezi Mungu basi hao ndio makafiri" [Maaida: 44] na "basi hao ndio madhalimu" [Maida: 45] na "basi hao ndio waovu" [Maida: 47], akasema: Amesema bin Abbasi: Aliziteremsha Mwenyezi Mungu kwa makundi mawili katika Mayahudi, na moja lilikuwa limelitenza nguvu jingine katika zama za ujinga, mpaka wakaridhiana na wakapatana kuwa kila dhalili aliyeuliwa na mtu mtukufu fidia yake ni Waski hamsini, sawa na (kg 6100), na kila maiti aliyeuliwa na mtu dhalili katika watukufu basi fidia yake ni Waski mia moja (100) sawa na (kg12,200), na walikuwa wakiishi katika maisha hayo mpaka alipokuja Mtume rehema na amani ziwe juu yake katika mji wa Madina, na makundi yote mawili yakajishusha kwa kufika Mtume rehema na amani ziwe juu yake, na Mtume rehema na amani ziwe juu yake wakati huo hajajulikana kwa watu, na hakuwa amewalazimisha na kuwatenza nguvu katika hilo, na huo ulikuwa ni wakati wa ule mkataba wa maridhiano (Hudaibia), basi mtu dhalili akamuuwa mtukufu mmoja, basi yule mtukufu akatuma ujumbe kwa ndugu wa yule dhalili kuwa tunataka mtuletee Waski mia moja (kg12,200) yule dhalili akasema: Je ni kweli ndivyo ilivyokuwa katika mitaa yao kwamba dini yao ni moja, na nasaba yao ni moja, na mji wao ni mmoja, kwamba fidia ya baadhi yao ni nusu ya wenzao? Bila shaka hakika sisi tumekupeni kiasi hicho kwa kutudhulumu, na kwakuwa tunawaogopa, ama kwakuwa Muhammadi amekuja hatutokupeni, basi vita ikakaribia kuwaka baina yao, kisha wakaridhiana kuwa wamfanye Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuwa muamuzi wao, kisha yule mtukufu akaanza kueleza na akasema: Wallahi Muhammadi hatokupeni toka kwao zaidi ya kile atakachowapa toka kwenu, na hakika wamesema kweli, hawakutupa isipokuwa kwa dhuluma na kwa kutuogopa sisi, na kuwatenza nguvu, basi tumeni kwa Muhammadi mtu atakayekuleteeni maoni yake: Ikiwa atakupeni mnachotaka basi mfanyeni kuwa hakimu wenu, na asipokupeni basi muepukeni na msimfanye kuwa hakimu, basi wakatuma kwenda kwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake watu miongoni mwa wanafiki ili wawaletee habari na maoni ya Mtume rehema na amani ziwe juu yake, walipofika kwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake, Mwenyezi Mungu alimpa habari Mtume wake ya jambo lao lote na kile walichokitaka, akateremsha Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Ewe Mtume! Wasikuhuzunishe wale ambao wanakimbilia kuukanusha unabii wako miongoni mwa wanafiki ambao wameonyesha Uislamu..." [Maida: 41] Mpaka katika kauli yake: "Na yeyote asiyehukumu kwa yale aliyoyateremsha Mwenyezi Mungu basi hao ndio mafasiki (waovu)" [Maida: 47] Kisha akasema kuhusu aya hizo, Wallah zimeteremka, na bila shaka wao ndio Mwenyezi Mungu Mtukufu aliwakusudia.
Explanation
Benefits
Vitimbi vya Mayahudi na dhuluma zao mpaka hata wao kwa wao.
Habari aliyoitoa Mwenyezi Mungu Mtukufu kuwa Mayahudi wana fedheha duniani na adhabu chungu Akhera.
Kutohukumu kwa yale aliyoyateremsha Mwenyezi Mungu na kuridhika na hukumu ya Mtume rehema na amani ziwe juu yake ni dalili ya ukafiri na dhulumu na uovu.
Hatari ya wanafiki na kusaidizana kwao na Mayahudi.
Attribution
Categories
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

