Ulimi wako usiache kuwa mbichi kwa kumtaja Mwenyezi Mungu
Choose an available translation of this Hadeeth
Hadeeth text
Kutoka kwa Abdallah bin Busri radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake amesema: Mtu mmoja alikuja kwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake, akasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu! Hakika sheria za Uislamu zimekuwa nyingi kwetu, ni mlango gani tushikamane nao uliokusanya mambo mengi? Akasema: "Ulimi wako usiache kuwa mbichi kwa kumtaja Mwenyezi Mungu". Na katika riwaya nyingine: Miongoni mwa hadithi za Muadhi radhi za Mwneyezi Mungu ziwe juu yake: Maneno ya mwisho niliochana na Mtume rehema na amani ziwe juu yake nilisema: Ni amali ipi bora na iko karibu zaidi na Mwenyezi Mungu? Akasema: "Ni ufe hali yakuwa ulimi wako ni mbichi kwa kumtaja Mwenyezi Mungu Aliyetakasika na Kutukuka".
Explanation
Mtume rehema na amani ziwe juu yake akamuelekeza kuwa ulimi wake uwe mbichi utikisike kwa kudumu kumtaja Mwenyezi Mungu Mtukufu kila wakati na kila hali; kama kumsabihi na kumhimidi na kumtaka msamaha na kumuomba na mfano wake.
Benefits
Miongoni mwa fadhila za Mwenyezi Mungu ni kufanya sababu za kupata malipo kuwa nyepesi.
Watu kuzidiana katika mafungu yao katika milango ya wema na kheri.
Kumtaja Mwenyezi Mungu kwa wingi kwa ulimi, kwa kumsabihi na kumhimidi, na kukiri kuwa hapana mola muabudiwa wa haki ila yeye, na kumtukuza, na mengineyo pamoja na moyo kwenda sambamba na ulimi, hili linakaa nafasi ya ibada nyingi za sunna.
Kuchunga kwake Mtume rehema na amani ziwe juu yake hali ya muulizaji kwa kumjibu kila linalomfaa.
Attribution
Categories
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

