الناس
An-Nas
Mankind
1 - An-Nas (Mankind) - 001
قُلۡ أَعُوذُ بِرَبِّ ٱلنَّاسِ
Sema: Ninajikinga kwa Mola Mlezi wa wanaadamu,
Sema: Najikinga na Mola Mlezi wa wanaadamu, Mwenye kuendesha mambo yao.
2 - An-Nas (Mankind) - 002
مَلِكِ ٱلنَّاسِ
Mfalme wa wanaadamu,
Mfalme wa wanaadamu, kwa ufalme ulio timia, kuwamiliki wote wafalme wao na maraia.
3 - An-Nas (Mankind) - 003
إِلَٰهِ ٱلنَّاسِ
Mungu wa wanaadamu,
Mungu wa wanaadamu, Mwenye uweza kwa kuwasarifu kwa ukamilifu atakavyo.
4 - An-Nas (Mankind) - 004
مِن شَرِّ ٱلۡوَسۡوَاسِ ٱلۡخَنَّاسِ
Na shari ya wasiwasi wa Shetani, Khannas,
Na shari ya mwenye kutia wasiwasi watu, ambaye hurudi nyuma ukiomba msaada kwa Mwenyezi Mungu dhidi yake.
5 - An-Nas (Mankind) - 005
ٱلَّذِي يُوَسۡوِسُ فِي صُدُورِ ٱلنَّاسِ
Anaye tia wasiwasi katika vifua vya watu,
Ambaye hutia kwa kificho katika vifua vya watu ya kuwaachisha wasende kwenye njia ya uwongofu.
6 - An-Nas (Mankind) - 006