Hakika kwako wewe kuna mambo mawili anayapenda sana Mwenyezi Mungu: Upole, na utaratibu
Imepokewa kutoka kwa Bin Abbas -radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na baba yake- amesema: Amesema Mtume rehema na amani ziwe juu yake kumwambia Ashajji Abdil-Kaisi: "Hakika kwako wewe kuna mambo mawili anayapenda sana Mwenyezi Mungu: Upole, na utaratibu".

