Nilimuuliza Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuhusu kutazama ghafla, akaniamrisha nigeuze jicho langu
Choose an available translation of this Hadeeth
Hadeeth text
Imepokelewa kutoka kwa Jariri bin Abdillah radhi za Allah ziwe juu yake amesema: Nilimuuliza Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuhusu kutazama ghafla, akaniamrisha nigeuze jicho langu.
Explanation
Benefits
Tahadhari ya kutazama kwa muda katika yale yaliyoharamishwa kuyatazama jicho linapodondokea ghafla na pasina kukusudia.
Ndani ya hadithi kuna uharamu kwa kuwatazama wanawake, jambo ambalo waliishi nalo Maswahaba, kwa ushahidi wa kuwa Jariri radhi za Allah ziwe juu yake alimuuliza Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuwa endapo litaangukia jicho lake katika kumtazama mwanamke pasina kukusudia, je hukumu yake itakuwa sawa na aliyekusudia kutazama?.
Na pia inaonyesha namna sheria ilivyotilia maanani masilahi ya waja, kwa kuwaharamishia kuwatazama wanawake, kwakuwa swala hilo linaambatana na maovu ya dunia na Akhera.
Kurejea Maswahaba kwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake na kumuuliza katika yale yanayowatatiza, na hivi ndivyo inavyotakiwa kwa watu wote kurejea kwa wanachuoni wao na kuwauliza katika yale yanayowatatiza.
Attribution
Categories
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

