Hakika katika yale waliyoyakuta watu miongoni mwa maneno ya kiutume ya mwanzo, usipokuwa na haya basi fanya ulitakalo
Choose an available translation of this Hadeeth
Hadeeth text
Kutoka kwa Abuu Masoud Uqba ni Amri Al-Answari Al-Badri radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake amesema: Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu: "Hakika katika yale waliyoyakuta watu miongoni mwa maneno ya kiutume ya mwanzo, usipokuwa na haya basi fanya ulitakalo".
Explanation
Benefits
Haya ni sifa miongoni mwa sifa za Manabii amani iwe juu yao, nayo ni katika mambo yaliyopokelewa kutoka kwao.
Haya ni ile inayomfanya muislamu kufanya yanayompa muonekano mzuri na wa kupendeza, na kuacha yanayomchafua na kuharibu muonekano.
Amesema Imam Nawawi: Amri iliyoko ndani yake ni ya uhalali, maana yake: Ukitaka kufanya jambo, ikiwa ni jambo ambalo hutoona haya kwa Mwenyezi Mungu au kwa watu, basi lifanye, vinginevyo usifanye, na huu ndio mwenendo wa Uislamu, na muongozo wa hayo ni kuwa amri zote na wajibu na sunna, ni aibu kuziacha, na yaliyokatazwa na haramu na haya ni aibu kuyafanya, na ama ya halali kuona haya kuifanya inajuzu, na vile vile kuiacha, Hadithi hii imekusanya hukumu tano, na imesemwa kuwa: Ni amri ya kutishia, na maana yake nikuwa: Iwapo staha itaondolewa, basi fanya chochote unachotaka; kwani Mwenyezi Mungu atakulipa kwa hilo, na ikasemwa kuwa: Ni amri kwa maana ya habari, maana yake: Asiyekuwa na haya anafanya apendavyo.
Attribution
Categories
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

