Atakayesimamia chochote kwa watoto wa kike hawa, akawatendea wema, basi watakuwa ni kinga kwake kutokana na moto
Choose an available translation of this Hadeeth
Hadeeth text
Kutoka kwa Aisha mama wa waumini radhi za Allah ziwe juu yake, mke wa Mtume rehema na amani ziwe juu yake, alimsimulia akasema: Alinijia mwanamke mmoja akiwa na watoto wake wawili akiniomba, nikawa sikupata ndani kwangu zaidi ya tende moja, nikampatia, akaigawanya baina ya watoto wake, kisha akanyanyuka akatoka, muda si mrefu, akaingia Mtume rehema na amani ziwe juu yake, akamsimulia kisa hicho, akasema: "Atakayesimamia chochote kwa watoto wa kike hawa, akawatendea wema, basi watakuwa ni kinga kwake kutokana na moto".
Explanation
Benefits
Sunna ya kutoa chochote kilicho ndani ya uwezo wa mtu hata kama ni kidogo.
Huruma kubwa ya wazazi kwa watoto wao.
Kumebainishwa hali ya nyumba za Mtume rehema na amani ziwe juu yake na kwamba riziki yake ilikuwa ya kumtosheleza pekee.
Kumebainishwa fadhila za kujinyima kwa ajili ya watu wengine, na kwamba hilo ni katika alama za waumini; kwani Aisha alimpendelea yule mwanamke na watoto wake kuliko nafsi yake, na hii inaonyesha juu ya ukarimu wake na moyo wake wa kujitolea pamoja na kuwa ana uvihitaji.
Zawadi ya watoto wa kike imeitwa kuwa ni mtihani; kwa sababu kuwalea kwake kuna shida na tabu nyingi, au kwa sababu ya baadhi ya watu kuwachukia, au ni kwa sababu mara nyingi wao huwa hawana vyanzo vya mapato ya maisha.
Uislamu ulikuja kung'oa mizizi ya desturi mbovu za zama za ujinga, na miongoni mwake nikuwa uliusia watu kuwalea vizuri watoto wa kike.
Mtu anapata malipo haya hata akiwa na binti mmoja kama ilivyokuja katika baadhi ya riwaya.
Attribution
Categories
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

