Karne bora ni karne yangu, kisha wale wanaowafuata, kisha wale wanaowafuata
Choose an available translation of this Hadeeth
Hadeeth text
Kutoka kwa Imrani bin Huswain radhi za Allah ziwe juu yake yeye na baba yake, amesema: Amesema Mtume rehema na amani ziwe juu yake: "Karne bora ni karne yangu, kisha wale wanaowafuata, kisha wale wanaowafuata" Amesema Imrani: Sijui alitaja Mtume rehema na amani ziwe juu yake baadaye karne mbili au tatu, akasema Mtume rehema na amani ziwe juu yake: "Hakika baada yenu kutakuja watu wanaofanya hiyana na wala hawaaminiwi, na wanatoa ushahidi na wala hawatakwi ushahidi, na wanatoa nadhiri na wala hawatimizi, na utadhihiri kwao unene".
Explanation
Benefits
Amesema bin Hajari: Na hadithi hii imepelekea Maswahaba kuwa bora zaidi kuliko wanafunzi wao (Matabii), na Matabii kuwa bora kuliko wanafunzi wao (Mataabii Taabiina), lakini je, ubora huu ni kulingana na ujumla wao au mtu mmoja mmoja? Hapa ni mahala pa kufanya utafiti, na kwa kauli hiyo ya pili ndio iliyochaguliwa na jopo la wanachuoni.
Ishara ya ulazima wa kufuata njia ya karne tatu za mwanzo; kwani kila ambaye zama zake zitakuwa karibu zaidi na zama za utume basi huyo ndiye anastahiki zaidi kuwa na fadhila na elimu na kuiga na kuongoka kutoka kwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake.
Nadhiri: Ni mtu mwenye ulazima wa kutekeleza sheria kuilazimisha nafsi yake kwa ibada ambayo sheria haikuifanya kuwa lazima kwa kila kauli iliyoielezea.
Ubaya wa hiyana na kutotimiza nadhiri na kufungamana na dunia.
Ubaya wa kutoa ushahidi pasina kutakwa kuutoa, ikiwa mwenye haki analijua hilo, na ama akiwa hajui linaingia katika kauli yake rehema na amani ziwe juu yake: "Hivi je nisikuelezeni mashahidi bora kuliko wote, ni yule anayetoa ushahidi kabla hajaulizwa" Kaipokea Muslim.
Attribution
Categories
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

