Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: Ananiudhi mimi mwanadamu, anatukana nyakati na mimi ndiye nyakati, ninaugeuza usiku na mchana
Choose an available translation of this Hadeeth
Hadeeth text
Imepokelewa kutoka kwa Abuu Huraira radhi za Allah ziwe juu yake amesema: Amesema Mtume rehema na amani ziwe juu yake: "Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: Ananiudhi mimi mwanadamu, anatukana nyakati na mimi ndiye nyakati, ninaugeuza usiku na mchana".
Explanation
Benefits
Kuwa na adabu na Mwenyezi Mungu Mtukufu katika kauli na itikadi.
Uwajibu wa kuamini maamuzi na mipango ya Mwenyezi Mungu, na kuwa na subira juu ya maudhi.
Maudhi si madhara; mwanadamu huudhika anaposikia mabaya au kuyaona; lakini hadhuriki kwa hilo, lakini pia anaudhika kwa harufu mbaya kama vitunguu maji na vitunguu thaumu na wala hadhuriki kwa hivyo.
Mwenyezi Mungu Aliyetakasika na kutukuka anaudhika kwa baadhi ya matendo mabaya ya waja wake, lakini yeye Aliyetakasika na kutukuka hadhuriki kwa hilo, kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu katika hadithil Kudsi: "Enyi waja wangu hakika nyinyi hamtofikia kunidhuru mkanidhuru, na wala hamtofikia kuninufaisha mkaninufaisha".
Kutukana zama na kuisifu kuna gawanyika katika sehemu tatu: 1- Ni atukane zama kuwa yenyewe ndiyo inayofanya hayo; na kwamba zama ndiyo zinazogeuza mambo kwenda katika kheri na shari! Hii ni shirki kubwa; kwa sababu hapa atakuwa kaitakidi kuwa kunamuumba mwingine pamoja na Mwenyezi Mungu, na ni kwa sababu ameambatanisha kupatikana kwa matukio na asiyekuwa Mwenyezi Mungu, 2- Ni atukane zama si kwa kuitakidi kwake kwamba zama ndio zinazotenda; bali anaitakidi kuwa Mwenyezi Mungu ndiye mtendaji lakini anaitukana kwa sababu ndio mahali pa maudhi haya kwake; hili ni haramu, 3- Akusudie kutoa habari bila kulaumu; hili linafaa, na katika hilo ni pamoja na kauli ya Lutu amani iwe juu yake: "Na akasema hii ni siku ngumu".
Attribution
Categories
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

