Mkimuomba Allah basi muombeni Firdausi
Choose an available translation of this Hadeeth
Hadeeth text
Kutoka kwa Ubaada bin Swaamit radhi za Allah ziwe juu yake hakika Mtume rehema na amani za Allah ziwe juu yake alisema: "Peponi kuna daraja mia moja baina ya kila daraja mbili ni kama umbali wa mbingu na ardhi, na Firdausi iko daraja ya juu zaidi kuliko zote, na ndani yake ndiko inako chimbuka mito yote minne ya pepo, na juu yake ndiko inakokuwa Arshi, Mkimuomba Allah basi muombeni Firdausi".
Explanation
Benefits
Himizo la kumuomba Mwenyezi Mungu Firdausi ya juu katika Pepo.
Firdausi ndiyo Pepo ya juu, na ndio bora zaidi kuliko zote.
Ni wajibu kwa muislamu hamu yake kuwa ya juu zaidi, na aende mbio na aombe makazi ya juu na bora zaidi kuliko yote mbele ya Mwenyezi Mungu Mtukufu.
Mito minne ya Pepo ni mito ya maji na maziwa na mvinyo na asali iliyotajwa ndani ya Qur'ani katika kauli yake Mtukufu: "Mfano wa Pepo waliyoahidiwa wachamungu, ndani yake kuna mito ya maji yasiyovunda, na mito ya maziwa isiyoharibika ladha yake, na mito ya mvinyo yenye ladha kwa wanywao, na mito ya asali iliyosafishwa" [Muhammadi: 15].
Attribution
Categories
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

