Hakika mchamungu wenu na mwenye kumjua zaidi Mwenyezi Mungu kwenu nyinyi ni mimi
Choose an available translation of this Hadeeth
Hadeeth text
Imepokelewa kutoka kwa Aisha mama wa waumini radhi za Allah ziwe juu yake amesema: Alikuwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake anapowaamrisha anawaamrisha katika matendo yale wanayoyaweza, wakasema: Sisi hatuna nafasi kama yako ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, hakika Mwenyezi Mungu amekusamehe yaliyotangulia katika madhambi yako na yajayo, basi anachukia mpaka anaonekana usoni kuwa amechukia, kisha anasema: "Hakika mchamungu wenu na mwenye kumjua zaidi Mwenyezi Mungu kwenu nyinyi ni mimi".
Explanation
Benefits
Mtu mwema hapaswi kuacha jitihada katika amali kwa kutegemea wema wake.
Inafaa mtu kusimulia neema alizonazo kulingana na haja ya kufanya hivyo, ikiwa atakuwa na uhakika wa kutojigamba au kujikweza.
Kilicho bora katika ibada ni kuwa kati na kati na kudumu, si kupita mpaka kunakopelekea kuacha.
Amesema bin Hajari: Mja anapofikia kiwango kikubwa katika ibada na matunda yake hilo kwake linakuwa ni msukumo wa kudumu nazo, ili kuzibakisha neema, na kuzizidisha kwa kushukuru.
Sheria ya kukasirika wakati wa kuvunjwa jambo la kisheria, na kumkemea mwerevu anayestahili kufahamu maana ya jambo endapo atashindwa kufahamu, ili kumchochea awe makini.
Huruma ya Mtume rehema na amani ziwe juu yake kwa Umma wake, na kwamba dini ni nyepesi, na sheria ni takasifu na yenye upole.
Hamu kubwa ya Maswahaba katika ibada, na kutaka kwao kuzidisha kufanya kheri.
Kusimama katika mipaka ya sheria katika wajibu na ruhusa, na kuamini kuwa kuchukua jepesi lenye kuendana na sheria ni bora kuliko gumu linalokwenda kinyume na sheria.
Attribution
Categories
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

