Hakika Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu na Mtukufu, halali, na wala haimstahikii kulala
Choose an available translation of this Hadeeth
Hadeeth text
Kutoka kwa Abuu Mussa radhi za Allah ziwe juu yake amesema: Alisimama kwetu Mtume rehema na amani ziwe juu yake kwa maneno matano, akasema: "Hakika Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu na Mtukufu, halali, na wala haimstahikii kulala, hushusha mizani ya uadilifu na huinyanyua, yanapandishwa kwake matendo ya usiku kabla ya matendo ya mchana, na matendo ya mchana kabla ya matendo ya usiku, pazia lake ni nuru, -na katika riwaya nyingine-: Lau kama angeliondoa, basi utukufu wa uso wake ungeunguza viumbe vyake mpaka pale ambapo macho yake yanafikia."
Explanation
Benefits
Mwenyezi Mungu Mtukufu anamtukuza amtakaye na anamdhalilisha amtakaye, na anamuongoza amtakaye na anampoteza amtakaye katika waja wake.
Matendo hunyanyuliwa kwa Mwenyezi Mungu kila mchana na usiku, na katika hilo kuna himizo kwa waja wamchunge Mwenyezi Mungu Aliyetakasika na kutukuka katika usiku wao na mchana wao.
Hadithi inaonyesha uadilifu wa Mwenyezi Mungu Mtukufu na uzuri wa upangiliaji wake wa mambo ya viumbe wake, na hakuna shaka kuwa hii ni katika sifa za ukamilifu wake Aliyetakasika na kuwa juu.
Kumethibitishwa pazia lake Aliyetakasika na kutukuka, nayo ni nuru inayokinga baina yake na baina ya viumbe wake, na lau isingekuwa hiyo wanageliungua.
Amesema Aajurri: Hakika watu wa haki humsifu Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa kile alichojisifu mwenye Mtukufu, na kwa kile alichomsifu nacho Mtume wake rehema na amani ziwe juu yake, na kwa kile walichomsifia Maswahaba radhi za Allah ziwe juu yao, na huu ndio msimamo wa wanachuoni katika wale walioamua kufuata sheria na hawakuzusha. Mwisho wa kunukuu. Watu wa sunna (wanaofuata mafundisho ya Mtume) wanamthibitishia Mwenyezi Mungu kile alichojithibitishia yeye mwenyewe katika majina na sifa, pasina kupotosha wala kukanusha wala kuuliza namna yake wala kupiga mfano, na wanamkanushia Mwenyezi Mungu yale aliyoyakanusha kwake, na wananyamaza kwa yale ambayo hayakukanushwa wala kuthibitishwa, amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Hakuna kitu kama mfano wake, na Yeye ni msikivu mwenye kuona".
Nuru ambayo ndiyo sifa yake Aliyetakasika na kutukuka si nuru ambayo amejikinga nayo, nuru aliyojikinga nayo imeumbwa, nuru ya Mwenyezi Mungu Mtukufu ni nuru inayoendana naye Yeye na dhati yake, hakuna kitu kama mfano wake, na alichokiona Mtume rehema na amani ziwe juu yake hakikuwa kingine zaidi ya pazia linalokuwa kati ya Mwenyezi Mungu na waja wake.
Attribution
Categories
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

