Hakika nyoyo za wanadamu zote ziko baina ya vidole viwili miongoni mwa vidole vya Rahmaan (Mwingi wa rehema), kama moyo wa mtu mmoja, anaugeuza kokote atakako
Choose an available translation of this Hadeeth
Hadeeth text
Imepokelewa kutoka kwa Abdullahi bin Amri bin Aaswi -radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na baba yake- amesema: Nilimsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu -rehema na amani ziwe juu yake akisema: "Hakika nyoyo za wanadamu zote ziko baina ya vidole viwili miongoni mwa vidole vya Rahmaan (Mwingi wa rehema), kama moyo wa mtu mmoja, anaugeuza kokote atakako" Kisha akasema Mtume rehema na amani ziwe juu yake: "Ewe Mwenyezi Mungu mwenye kuzigeuza nyoyo, zigeuze nyoyo zetu zielekee katika kukutii".
Explanation
Benefits
Inampasa muislamu kudumu kumuomba Mola wake Mlezi kuthubutu katika haki na uongofu.
Kumhofu Mwenyezi Mungu na kufungamana nayeye peke yake asiye na mshirika.
Amesema Aajurri: Hakika watu wa haki humsifu Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa sifa alizojisifu mwenyewe Aliyetakasika na kutukuka, na kwa sifa alizomsifu kwazo Mtume wake rehema na amani ziwe juu yake, na kwa zile walizomsifu kwazo Maswahaba radhi za Allah ziwe juu yao, na huu ndio msimamo wa wanachuoni katika wale waliofuata muongozo na wala hawakuzua. Mwisho. Watu wa sunna humthibitishia Mwenyezi Mungu aliyoyathibitisha yeye mwenyewe kwa nafsi yake katika majina na sifa pasina kupotoa, wala kukanusha wala kuhoji wala kufananisha, na wanamkanushia Mwenyezi Mungu yale aliyoyakanusha yeye mwenyewe juu nafsi yake, na wananyamaza katika yale ambayo mafundisho hayakueleza kuthibitisha au kukanusha, amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Hakuna chochote mfano wake, naye ni Msikivu Mwenye kuona".
Attribution
Categories
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

