Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi najikinga kwako kutokana na kushindwa, na uvivu, na uoga, na ubahili, na ukongwe, na adhabu ya kaburi, Ewe Mwenyezi Mungu ipe nafsi yangu uchamungu wake, na uitakase kwani wewe ndiye mbora wa kuitakasa, wewe ndiye msimamizi wa nafsi na mtawala wake. Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi ninajikinga kwako kutokana na elimu isiyo na manufaa, na moyo usiyo nyenyekea, na nafsi isiyo tosheka, na maombi yasiyo jibiwa
Choose an available translation of this Hadeeth
Hadeeth text
Kutoka kwa Zaidi bin Arqam radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake amesema: Sikwambieni isipokuwa kama alivyokuwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake akisema: Alikuwa akisema: "Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi najikinga kwako kutokana na kushindwa, na uvivu, na uoga, na ubahili, na ukongwe, na adhabu ya kaburi, Ewe Mwenyezi Mungu ipe nafsi yangu uchamungu wake, na uitakase kwani wewe ndiye mbora wa kuitakasa, wewe ndiye msimamizi wa nafsi na mtawala wake. Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi ninajikinga kwako kutokana na elimu isiyo na manufaa, na moyo usiyo nyenyekea, na nafsi isiyo tosheka, na maombi yasiyo jibiwa".
Explanation
Benefits
Himizo juu ya uchamungu na kusambaza elimu na kuifanyia kazi.
Elimu yenye manufaa inayoitakasa nafsi na kuizalishia hofu ya Mola Mlezi Aliyetakasika na kutukuka, na kutiririka katika viungo vingine vilivyobakia.
Moyo wenye unyenyekevu ni ule unaoogopa na kutaharuki wakati wa kutajwa Mwenyezi Mungu kisha ukalainika na kutulia.
Chukizo la kuipupia dunia na kutoshiba kutokana na matamanio yake na ladha zake, na ndio maana nafsi inayotokota yenye pupa na starehe za dunia ndio adui mkubwa wa mtu, na ndio maana alijikinga dhidi yake Mtume rehema na amani ziwe juu yake.
Inampasa mja ajitenge mbali na sababu za kukataliwa dua na kutojibiwa kwake.
Amesema Nawawi: Hadithi hii na nyinginezo ni miongoni mwa dua zenye vina, ni ushahidi waliousema wanachuoni; kuwa vina visivyotakiwa katika dua ni vile vya kujikalifisha, kwani huondoa utulivu na unyenyekevu na utakasifu, na hupumbaza na kuacha kujinyenyekeza na moyo kuwa mtupu, ama inayofanyika bila kujikalifisha wala kushughulisha akili kwa sababu ya ukamilifu wa ufasaha na mfano wake, au ikawa mtu kaihifadhi, hii haina ubaya, bali ndio nzuri.
Attribution
Categories
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

