Imenyanyuliwa kalamu kwa watu wa aina tatu: Kwa aliyelala mpaka aamke, na kwa mtoto mdogo mpaka abalehe, na kwa mwendawazimu mpaka apate akili
Choose an available translation of this Hadeeth
Hadeeth text
Imepokelewa kutoka kwa Othman -radhi za Allah ziwe juu yake- kutoka kwa Mtume -rehema na amani ziwe juu yake- amesema: "Imenyanyuliwa kalamu kwa watu wa aina tatu: Kwa aliyelala mpaka aamke, na kwa mtoto mdogo mpaka abalehe, na kwa mwendawazimu mpaka apate akili".
Explanation
Mtoto mdogo mpaka akue na abalehe.
Na kwa mwendawazimu aliyepoteza akili mpaka akili irudi.
Na kwa aliyelala mpaka aamke.
Kubeba wajibu kumeondolewa kwao, na kutenda kwao madhambi hakuandikwi, lakini mtoto huandikiwa kheri anapofanya, isipokuwa mwendawazimu na aliyelala; kwa sababu wote hawa wako katika kundi la mtu asiyekubalika ibada yake kwa kupoteza hisia.
Benefits
Kutoandika dhambi zao hakufuti baadhi ya hukumu za kidunia dhidi yao; kama mwendawazimu akiua, hakuna kisasi wala kafara kwake, na mtu wake mwenye akili timamu lazima alipe fidia.
Kubalehe kuna dalili tatu: Kutokwa na manii, kwa kujiotea au kwa kinginecho, au kuota nywele sehemu za siri, au kutimiza miaka kumi na tano, na linaongezeka jambo la nne kwa mwanamke: nalo ni hedhi.
Amesema Al-Subki: Mtoto kijana, na wengine wakasema: Mtoto aliye tumboni mwa mama yake anaitwa kijusi, akizaliwa anaitwa mvulana, na akiachishwa kunyonya, basi ni mvulana mpaka saba, basi anakuwa kijana mpaka kumi, kisha mdogo hadi kumi na tano, na kilicho yakini ni kwamba anaitwa mvulana katika matukio yote haya, alisema Al-Suyuti.
Attribution
Categories
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

