Atakayekuwa na wake wawili akaegemea kwa mmoja wao atakuja siku ya Kiyama upande wake mmoja ukiwa umepinda
Choose an available translation of this Hadeeth
Hadeeth text
Imepokelewa kutoka kwa Abuu Huraira -radhi za Allah ziwe juu yake- kutoka kwa Mtume -rehema na amani ziwe juu yake- amesema: "Atakayekuwa na wake wawili akaegemea kwa mmoja wao atakuja siku ya Kiyama upande wake mmoja ukiwa umepinda".
Explanation
Benefits
Kufanya usawa katika mgao na mfano wa hayo, katika yale anayoyamiliki mtu, ama yale asiyoyamiliki kama mapenzi na kuegemea kwa moyo, hayo hayaingii katika hadithi, na ndio yaliyokusudiwa katika kauli yake Mtukufu: "Na kwamwe hamtoweza kutenda uadilifu kati ya wanawake hata mkifanya pupa (juu ya hilo) [An-Nisaa: 129].
Malipo huendana na namna ya matendo, kwa sababu mwanaume alipoegemea upande mmoja duniani kwa mwanamke mmoja akamuacha mwingine, atakuja siku ya Kiyama moja kati pande zake ukiwa umepinda umepishana na mwingine.
Kuheshimu haki za waja, nakuwa haki hizo hazisameheki; kwa sababu zimejengeka katika uchoyo na kulipizana.
Inapendeza kuishia mke mmoja, mwanaume akihofia kutowatendea uadilifu wake zake; ili asiangukie katika madhaifu katika dini; amesema Mtukufu: "Ikiwa mtahofia kutowafanyia uadilifu basi (bakini na) mmoja" [An-Nisaa: 3].
Attribution
Categories
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

