Atakayekuwa na dhuluma yoyote ya ndugu yake kama heshima au chochote, basi na wamalizane leo hii, kabla ya wakati ambao hapatakuwa na Dinar wala Dirham
Choose an available translation of this Hadeeth
Hadeeth text
Imepokelewa kutoka kwa Abuu Huraira radhi za Allah ziwe juu yake amesema: Amesema Mtume -rehema na amani ziwe juu yake: "Atakayekuwa na dhuluma yoyote ya ndugu yake kama heshima au chochote, basi na wamalizane leo hii, kabla ya wakati ambao hapatakuwa na Dinar wala Dirham, ikiwa atakuwa na amali njema basi zitachukuliwa kwake kwa kiasi cha dhuluma yake, na akiwa hana mema basi yatachukuliwa maovu ya mwenye haki na atabebeshwa yeye".
Explanation
Benefits
Himizo la kufanya haraka kujiondoa katika dhima (haki za watu) katika zile alizonazo miongoni mwa haki.
Matendo mema huharibiwa na kutoweka tija yake kwa kuwadhulumu watu na kuwaudhi.
Haki za watu hazisamehi Mwenyezi Mungu isipokuwa kwa kuzirejesha kwa wenye nazo.
Dinar na Dirham ni njia za kuleta manufaa katika Dunia, ama siku ya Kiyama ni matendo mema na maovu pekee.
Wamesema baadhi ya wanachuoni katika maswala ya heshima: Ikiwa aliyedhulumiwa hakujua kama alivunjiwa heshima yake, hakuna haja ya kumjulisha, mfano kama alimtukana katika kikao miongoni mwa vikao na akatubia, basi haina haja ya kumwambia, lakini anatakiwa amuombee msamaha na amuombee mazuri pia, na amtaje kwa mazuri katika kikao hicho hicho alichokuwa akimtukana ndani yake, na kwa kufanya hivyo atakuwa kajivua na hilo.
Attribution
Categories
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

