Hivi nisikuelezeni watu wa peponi? Kila mnyonge mwenye kujishusha, na lau kama angeliapia kwa Mwenyezi Mungu basi angelimuepusha (na kutopokea kiapo chake), hivi nisikuelezeni watu wa motoni? kila jeuri mkaidi mwenye kiburi
Choose an available translation of this Hadeeth
Hadeeth text
Kutoka kwa Haritha bin Wahabi Al-Khuzaai radhi za Allah ziwe juu yake amesema: Nilimsikia Mtume rehema na amani ziwe juu yake akisema: "Hivi nisikuelezeni watu wa peponi? Kila mnyonge mwenye kujishusha, na lau kama angeliapia kwa Mwenyezi Mungu basi angelimuepusha (na kutopokea kiapo chake), hivi nisikuelezeni watu wa motoni? kila jeuri mkaidi mwenye kiburi".
Explanation
Asilimia kubwa ya watu wa peponi ni: "Kila mnyonge mwenye kujishusha", yaani: Mnyenyekevu mwenye kujishusha kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu, mwenye kuidhalilisha nafsi yake kwake, mpaka baadhi ya watu wakamdhoofisha na kumdharau, na huyu mwenye kujidhalilisha kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu lau kama ataapa kwa Mwenyezi Mungu kiapo cha kutamani jambo katika karama za Mwenyezi Mungu Mtukufu, basi Mwenyezi Mungu angemuepusha na kutopokea kiapo chake, na angelimtimizia alichokiapia na angelijibu ombi lake na dua yake.
Na asilimia kubwa ya watu wa motoni ni: Kila "Mkaidi" Naye ni fidhuli mkorofi mwingi wa ugomvi, au muovu asiyetii kwa kufata jambo la kheri, "Jeuri" Naye ni mwenye kiburi, mlafi, mwenye mwili mkubwa, mwenye kutembea kwa maringo, mwenye tabia mbaya, "Mwenye kufanya kiburi" kwa kuikataa kwake haki, na kwa kumdharau mtu mwingine.
Benefits
Unyenyekevu unakuwa kwa Mwenyezi Mungu Aliyetakasika na kutukuka, na kwa amri zake na makatazo yake na kutii, na unakuwa kwa viumbe kwa kutojikweza juu yao.
Amesema bin Hajari: Makusudio yake nikuwa asilimia kubwa ya watu wa peponi ni hawa, kama ambavyo watu wengi wa motoni ni sehemu hii nyingine, na wala makusudio yake si kueleza watu wote wa motoni watakuwa na sifa hizi.
Attribution
Categories
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

