Mwenye kumuamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho basi na aseme la kheri au anyamaze
Choose an available translation of this Hadeeth
Hadeeth text
Imepokewa kutoka kwa Abuu Huraira -Allah amridhie- kutoka kwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- amesema: "Mwenye kumuamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho basi na aseme la kheri au anyamaze, na mwenye kumuamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho basi na amkirimu jirani yake, na mwenye kumuamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho basi na amkirimu mgeni wake".
Explanation
La kwanza: Kauli njema: Kama tasbihi (kusema: Sub-haanallah) na tahlili (Laa ilaaha illa llaah) na kuamrisha mema, na kukataza mabaya, na kuwasuluhisha watu, ikiwa hatofanya hivyo basi ashikamane na ukimya, na ajizuie na maudhi yake, na ahifadhi ulimi wake.
La pili: Kumkirimu jirani: Kwa kumtendea wema na kutomuudhi.
La tatu: Kumkirimu mgeni anayekuja kukutembelea: Kwa maneno mazuri na kumlisha chakula na mfano wa hayo.
Benefits
Tahadhari dhidi ya maafa ya ulimi.
Dini ya Uislamu ni dini ya ukaribu na ukarimu.
Mambo haya ni katika vipengele vya imani na ni katika adabu njema.
Maneno mengi yanayeweza kumvuta mtu katika machukizo au uharamu, na kusalimika na hilo ni kutozungumza ila katika kheri.
Attribution
Categories
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

