Enyi waja wangu hakika Mimi nimeharamisha dhulma juu ya Nafsi yangu na nikaifanya kuwa ni haramu baina yenu, basi msidhulumiane
Choose an available translation of this Hadeeth
Hadeeth text
Imepokewa kutoka kwa Abuu Dharri -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake-: Kutoka kwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake-katika yale aliyoyapokea kutoka kwa Mola wake Mtukufu hakika Yeye amesema: "Enyi waja wangu hakika Mimi nimeharamisha dhulma juu ya Nafsi yangu na nikaifanya kuwa ni haramu baina yenu, basi msidhulumiane, enyi waja wangu nyote ni wapotevu isipokuwa yule niliye muongoza, basi niombeni uongofu nami nitakuongozeni, enyi waja wangu nyote ni wenye njaa isipokuwa yule niliye mlisha, basi niombeni chakula nami nitakulisheni, enyi waja wangu nyote mpo uchi isipokuwa yule niliye mvisha, basi niombeni kuvaa nami nitakuvisheni, enyi waja wangu hakika nyinyi mnakosea usiku na mchana na mimi ninasamehe madhambi yote, basi niombeni msamaha nami nitakusameheni, enyi waja wangu hamtafikia kufanya madhara ili mnidhuru wala hamtafanya mambo yenye manufaa ili mninufaishe, enyi waja wangu laiti wa mwanzo wenu na wa mwisho wenu binadamu na majini wakijikusanya wote wakawa na ucha Mungu wa mtu mmoja hilo lisinge niongezea chochote katika Ufalme wangu chochote, enyi waja wangu laiti wa mwanzo wenu na wa mwisho wenu binadamu na majini wakijikusanya wote wakafanya uovu wa mtu mmoja hilo lisinge punguza chochote katika Ufalme wangu, enyi waja wangu laiti wa mwanzo wenu na wa mwisho wenu binadamu na majini wangejikusanya katika uwanja mmoja wakaniomba nikampa kila mtu alicho kiomba hilo lisinge punguza chochote katika Ufalame wangu isipokuwa ni kama sindano inavyo punguza maji pindi inapo ingizwa baharini, enyi waja wangu si vinginevyo bali hakika matendo yenu yote nina wahifadhieni kisha nitawapa malipo yenu, mwenye kupata kheri amshukuru Mwenyezi Mungu, na atakayepata kinyume na hayo basi asimlaumu yeyote isipokuwa nafsi yake."
Explanation
Nakuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu anayahifadhi matendo ya waja na kisha anawatunzia, kisha anawatimizia malipo siku ya Kiyama, atakayekuta malipo ya matendo yake yakiwa ni kheri basi na amshukuru Mwenyezi Mungu kwa kumuafikisha kwake katika kumtii, na atakayekuta malipo ya matendo yake ni kinyume na hivyo basi asilaumu ila nafsi yake yenye kuamrisha maovu iliyompelekea katika hasara.
Benefits
Kinachotokea kwa waja kwanzia elimu au kuongoka, ni kwa muongozo wa Mwenyezi Mungu na elimu yake.
Haimpati mja kheri yoyote isipokuwa inatoka kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu, na haimpati shari isipokuwa inatoka katika nafsi yake na matamanio yake.
Atakayefanya vizuri basi ni kwa taufiki ya Mwenyezi Mungu, na malipo yake ni fadhila kutoka kwa Mwenyezi Mungu, hivyo anastahiki sifa, na atakayefanya uovu basi asilaumu ila nafsi yake.
Attribution
Categories
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

