Fanyeni matendo na muwe na msimamo, na tambueni kuwa hatosalimika mmoja wenu kwa sababu ya matendo yake, wakasema: Hata wewe ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu?! Akasema: Hata mimi isipokuwa atakaponifunika mimi Mwenyezi Mungu kwa huruma zake na fadhila zake
Choose an available translation of this Hadeeth
Hadeeth text
Imepokelewa kutoka kwa Abuu Huraira -radhi za Allah ziwe juu yake- amesema: Amesema Mtume -rehema na amani ziwe juu yake-: "Fanyeni matendo na muwe na msimamo, na tambueni kuwa hatosalimika mmoja wenu kwa sababu ya matendo yake, wakasema: Hata wewe ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu?! Akasema: Hata mimi isipokuwa atakaponifunika mimi Mwenyezi Mungu kwa huruma zake na fadhila zake".
Explanation
Kisha akawaeleza kuwa amali hazitomuokoa yeyote miongoni mwao kamwe; bali ni lazima kuwe na rehema ya Mwenyezi Mungu.
Wakasema: Hata wewe ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu hazitokuokoa amali zako pamoja na ukubwa wa kiwango chake?
Akasema: Hata mimi, ila kama atanisitiri Mwenyezi Mungu kwa fadhila na rehema zake.
Benefits
Amesema bin Bazi: Matendo mema ndio sababu ya kuingia peponi, kama ambavyo matendo machafu ni sababu ya kuingia motoni, na hadithi inabainisha kuwa kuingia peponi si tu kwa kufanya matendo pekee, bali ni lazima kuwe na msamaha wa Mwenyezi Mungu na rehema yake Aliyetakasika na kutukuka, hivyo kuingia kwao ni kwa sababu ya matendo yao, lakini kinachowajibisha hilo ni rehema yake Mtukufu, na msamaha wake na maghufira yake.
Mja ahadaiki na kujifaharisha kwa matendo yake vyovyote vile yatavyofikia; kwa sababu haki ya Mwenyezi Mungu ni kubwa kuliko amali yake, ni lazima amali iwe na hofu na kutaraji rehema, vyote kwa pamoja.
Fadhila za Mwenyezi Mungu na rehema zake kwa waja wake ni pana kuliko amali zao.
Matendo mema ni sababu ya kuingia peponi, na kufuzu kuipata ni kwa fadhila za Mwenyezi Mungu na rehema kutoka kwake.
Amesema Al-Karmaani: "Ikiwa watu wote hawatoingia peponi ila kwa rehema ya Mwenyezi Mungu, hivyo namna ya kumhusisha Mtume rehema na amani ziwe juu yake kwa kumtaja kuwa hatoingia peponi ila kwa rehema ya Mwenyezi Mungu pamoja nakuwa kapewa uhakika wa kuingia peponi, hii inamaanisha kuwa mtu mwingine asiyekuwa yeye ndio ana haki zaidi ya kutoingia ila kwa rehema yake Mwenyezi Mungu.
Amesema Imam Nawawi: Katika maana ya kauli yake Mtukufu: "Ingieni peponi kwa sababu ya yale mliyokuwa mkiyafanya" [An Nahl: 32], "Na hiyo pepo mliyorithishwa ni kwa sababu ya yale mliyokuwa mkiyafanya" [Az-Zukhruf: 72] Na mifano mingine ya aya kama hizi zinazoonyesha kuwa matendo yatampeleka mtu peponi, hazipingani na hadithi hii, bali maana ya aya hizi nikuwa kuingia peponi ni kwa sababu ya matendo kisha kupata taufiki ya matendo hayo, na kuongozwa katika Ikhlasi ndani yake, na kukubalika kwake ni kwa rehema ya Mwenyezi Mungu Mtukufu na fadhila zake, hapa itakubalika kusema kuwa mtu hajaingia peponi kwa matendo pekee, na inasihi kusema kuwa kaingia kwa matendo: Yaani kwa sababu yake, nayo pia ni katika rehema.
Amesema bin Jauzi: Hapa yanapatikana majibu manne: La kwanza: Nikuwa kupata taufiki ya kutenda amali njema ni katika rehema za Mwenyezi Mungu, na lau kama si rehema za Mwenyezi Mungu zilizotangulia isingepatikana imani wala utiifu ambao ndio sababu ya kuokoka. La pili: Nikuwa manufaa ya mtumwa yapo kwa bosi wake hivyo matendo yake ni haki stahiki ya bwana wake, vyovyote vile atakavyomneemesha kwa malipo yote hayo ni katika fadhila zake. La tatu: Imekuja katika baadhi ya hadithi kuwa hata kuingia pepo kwenyewe pia ni katika rehema za Mwenyezi Mungu, na mgawanyo wa madaraja utakuwa kwa mujibu wa matendo. La nne: Nikuwa matendo ya utiifu yalikuwa kwa muda mfupi, na thawabu hazimaliziki, kuneemeshwa ambako hakumaliziki kupitia matendo yanayomalizika hii ni kwa sababu ya fadhila wala si kwa kulinganisha na matendo.
Amesema Ar-Raafii: Nikuwa, mfanyaji hatakiwi kubweteka katika amali zake katika kutafuta kusalimika na kuzipata daraja za juu; kwa sababu alifanya mema kwa taufiki ya Mwenyezi Mungu na aliacha maasi kwa hifadhi ya Mwenyezi Mungu, yote ni kwa fadhila zake na rehema zake.
Attribution
Categories
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

