Hivi kwani hajakuwekeeni Mwenyezi Mungu mambo mnayoweza kutoa sadaka: Hakika katika kila tasbihi (kauli ya sub-haanallaah) ni sadaka, na kila takbira (Allahu Akbaru) ni sadaka, na kila tahmidi (Alhamdulillah) ni sadaka, na kila tahalili (Laa ilaaha illallaahu) ni sadaka, na kuamrisha mema ni sadaka, na kukataza maovu ni sadaka, na katika kiungo cha siri cha mmoja wenu kuna sadaka
Choose an available translation of this Hadeeth
Hadeeth text
Imepokelewa kutoka kwa Abuu Dharri -radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake-: Yakwamba watu miongoni mwa Maswahaba wa Mtume rehema na amani ziwe juu yake walisema kumwambia Mtume rehema na amani ziwe juu yake. Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, wamechukua malipo mengi wenye utajiri: Wanaswali kama tunavyoswali na wanafunga kama tunavyofunga, na wanatoa sadaka katika mali yao ya akiba. Akasema: Hivi kwani hajakuwekeeni Mwenyezi Mungu mambo mnayoweza kutoa sadaka: Hakika katika kila tasbihi (kauli ya sub-haanallaah) ni sadaka, na kila takbira (Allahu Akbaru) ni sadaka, na kila tahmidi (Alhamdulillah) ni sadaka, na kila tahalili (Laa ilaaha illallaahu) ni sadaka, na kuamrisha mema ni sadaka, na kukataza maovu ni sadaka, na katika kiungo cha siri cha mmoja wenu kuna sadaka" Wakasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, hivi yawezekanaje akidhi mmoja wetu matamanio yake kisha awe na malipo? Akasema: Mnasemaje ikiwa atakiweka katika haramu, je atakuwa na mzigo wa dhambi? basi ndivyo hivyo akikiweka katika halali atakuwa na malipo".
Explanation
Benefits
Kukithiri kwa njia za amali za kheri, nakuwa zinakusanya kila amali anayoifanya muislamu kwa nia njema na lengo zuri.
Urahisi wa Uislamu na wepesi wake, kila muislamu anapata anayoweza kuyafanya ili amtii Mwenyezi Mungu kwayo.
Amesema Nawawi: Na katika hili kuna dalili yakuwa mambo ya halali yanaweza kuwa ibada kwa nia ya kweli, tendo la ndoa linakuwa ibada atakaponuia kukidhi haki ya mke na kushiriki naye kwa wema ambao ameamrishwa na Mwenyezi Mungu Mtukufu, au kutafuta mtoto mwema, na kuilinda nafsi yake na nafsi ya mke wake na kujizuia wote wawili na kutazama haramu, au kuifikiria, au kutamani kufanya, au mengineyo katika malengo mazuri.
Amepiga mfano na kupima kwa akili; ili jambo liwe wazi na liingie vizuri ndani ya nafsi ya msikilizaji.
Attribution
Categories
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

