Pindi nilipopandishwa juu mbinguni, nilipita kwa watu wakiwa na kucha za shaba, wakizikwarua kwazo nyuso zao na vifua vyao
Choose an available translation of this Hadeeth
Hadeeth text
Imepokelewa kutoka kwa Anas radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake amesema: Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu -rehema na amani ziwe juu yake: "Pindi nilipopandishwa juu mbinguni, nilipita kwa watu wakiwa na kucha za shaba, wakizikwarua kwazo nyuso zao na vifua vyao, nikasema: Ni akina nani hao ewe Jibrili, akasema: Hawa ni wale wanaokula nyama za watu, na wanajitumbukiza katika kuvunja heshima za watu".
Explanation
Benefits
Kutia dosari heshima za watu ni katika kuwasengenya na mfano wake ni katika madhambi makubwa.
Amesema Attwayibi: Katika kauli yake: "Wakizikwarua", Amesema: Kwa sababu kukwarua uso na kifua ni miongoni mwa sifa za wanawake wanaoomboleza kwa mayowe, basi Mwenyezi Mungu akazifanya kuwa ndio malipo ya mwenye kusengenya na kuchafua heshima za Waislamu, akionyesha kuwa hizo si katika sifa za wanaume, bali hizo ni katika sifa za wanawake wakiwa katika hali mbaya zaidi na sura mbaya mno.
Uwajibu wa kuamini ghaibu na yale yote aliyoyaeleza Mwenyezi Mungu na Mtume wake rehema na amani ziwe juu yake.
Attribution
Categories
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

