HadeethEnc · 1.18.0
Utakapomwambia mwenzako: Nyamaza, siku ya Ijumaa, na imamu akihutubu, basi utakuwa umefanya mchezo
Available translations
Choose an available translation of this Hadeeth
01
Hadeeth text
Imepokelewa kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Allah ziwe juu yake- yakwamba Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- amesema: "Utakapomwambia mwenzako: Nyamaza, siku ya Ijumaa, na imamu akihutubu, basi utakuwa umefanya mchezo".
02
Explanation
Anabainisha Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kuwa katika adabu za wajibu kwa atakayehudhuria hotuba ya Ijumaa: Ni kunyamaza na kumsikiliza hatibu; ili mtu azingatie mawaidha, nakuwa atakayezungumza walau kwa jambo dogo, na imamu akihutubu, akasema kumwambia mwenzie: "Nyamaza" na "Sikiliza", basi zitakuwa zimempita fadhila za swala ya Ijumaa.
03
Benefits
Uharamu wa mazungumzo wakati wa hotuba, hata kama ni kuzia uovu au kujibu salamu au kumuombea dua aliyepiga chafya.
Anaondolewa katika katazo hili atayemsemesha imamu au imamu akamsemesha yeye.
Inafaa kuzungumza kati ya hotuba mbili.
Akitajwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- na imamu akiwa katika hotuba basi unatakiwa kumswalia kwa siri, na hivyo hivyo kuitikia dua.
Anaondolewa katika katazo hili atayemsemesha imamu au imamu akamsemesha yeye.
Inafaa kuzungumza kati ya hotuba mbili.
Akitajwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- na imamu akiwa katika hotuba basi unatakiwa kumswalia kwa siri, na hivyo hivyo kuitikia dua.
Attribution
[Wamekubaliana Bukhari na Muslim juu ya usahihi wake]
Categories
Share
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

