Yeyote atakayetoa kiapo hali yakuwa ni muongo, ili ajikatie mali ya mtu Muislamu, basi atakutana na Mwenyezi Mungu akiwa kamkasirikia
Choose an available translation of this Hadeeth
Hadeeth text
Kutoka kwa Abdallah bin Masoud radhi za Allah ziwe juu yake amesema: Amesema Mtume rehema na amani ziwe juu yake: "Yeyote atakayetoa kiapo hali yakuwa ni muongo, ili ajikatie mali ya mtu Muislamu, basi atakutana na Mwenyezi Mungu akiwa kamkasirikia". Akasema: Akasema Al-Ash'athi: Kwangu mimi Wallahi kulitokea tukio hilo; kulikuwa na Ardhi baina yangu na bwana mmoja Yahudi, akanipinga kuwa si yangu, nikampeleka kwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake akasema Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuniambia: "Je una ushahidi?" Nikasema: Hapana: Akasema kumwambia Yahudi: "Toa kiapo". Anasema: Nikasema ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, sasa si ataapa na atachukua mali yangu!. Akateremsha Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Hakika wale wanaouza ahadi ya Mwenyezi Mungu na viapo vyao kwa thamani ndogo..." mpaka mwisho wa aya.
Explanation
Benefits
Uzito wa haki za waislamu katika kidogo na kingi.
Ushahidi kwa mwenye kudai, na kiapo kwa mlalamikiwa atakapokataa.
Haki inathibiti kwa mashahidi wawili, usipopatikana ushahidi kwa mlalamikaji, basi ni lazima kwa mlalamikiwa kutoa kiapo.
Uharamu wa kiapo cha (kuzama) nacho ni kiapo cha uongo ambacho muapaji anajikatia haki ya mtu mwingine, nalo ni katika madhambi makubwa, ambalo linamtia mtu katika ghadhabu za Mwenyezi Mungu Mtukufu na adhabu zake.
Nasaha za hakimu wakati wa mzozo, hasa hasa wakati wa kutaka kiapo.
Attribution
Categories
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

