MAFUNZO MUHIMU KWA UMMAH MZIMA

Kitabu kwa lugha ya kiswahili amekitunga Dr.Haytham Sarhaan nayo ni sherhe ya matni ya الدروس المهمة لعامة الامة ya imaam ibn baaz Rahimahu llaah
Amekusanya ndani mkusanyiko wa elimu za kisheria zenye kuhusiana na hukmu za kifiqhi na aqida na tabia ambazo inapasa watu wote wazifahamu.

Amekiweka mtunzi katika mpangilio mzuri wa majedwali na mafungu, ametaja ndani yake makusudio na maana za ujumla na akaweka baada ya kila kifungu maswali na mitihani, yote hayo pasi na ufupi wenye mapungufu wala urefu wenye kuchosha.