Hakika ilikuwa inakutosheleza kupiga kwa mikono yako hivi" Kisha akapiga kwa mikono yake miwili chini ya ardhi mpigo mmoja, kisha ukapaka mkono wa kushoto juu ya mkono wa kulia, na juu ya viganja vyake na uso wake
Kutoka kwa Ammari Bin Yasiri radhi za Allah ziwe juu yake amesema: Aliniagiza Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- katika haja fulani, nikapatwa na janaba, nikawa sikupata maji, nikajigaragaza katika udongo kama anavyojigaragaza mnyama, kisha nikamuendea Mtume -Rehema…

