HadeethEnc · 1.18.0
Atakayeandaa mnyama kwa ajili ya kuchinja, na ukaandama mwandamo wa mwezi Dhul Hija, basi asipunguze chochote katika nywele zake wala kucha zake mpaka atakapochinja mnyama wake wa Udh-hiya
Available translations
Choose an available translation of this Hadeeth
01
Hadeeth text
Kutoka kwa Ummu Salama mama wa waumini mke wa Mtume rehema na amani ziwe juu yake radhi za Allah ziwe juu yake amesema: Amesema Mtume rehema na amani ziwe juu yake: "Atakayeandaa mnyama kwa ajili ya kuchinja, na ukaandama mwandamo wa mwezi Dhul Hija, basi asipunguze chochote katika nywele zake wala kucha zake mpaka atakapochinja mnyama wake wa Udh-hiya"
02
Explanation
Amemuamrisha Mtume rehema na amani ziwe juu yake atakayetaka kuchinja Udh-hiya asipunguze chochote katika nywele za kichwa chake au kwapa yake au sharubu zake au zinginezo, wala sehemu ya kucha za mikono yake wala miguu yake utakapoonekana mwandamo wa Dhul-Hija mpaka atakapochinja.
03
Benefits
Atakayenuia kuchinja baada ya kuingia siku kumi basi aanze kujizuia kulikoelezwa kwanzia wakati aliponuia mpaka atakapochinja.
Asipochinja katika siku ya kwanza, ataendelea kujizuia mpaka atakapochinja katika siku yoyote miongoni mwa siku za kubanika nyama.
Asipochinja katika siku ya kwanza, ataendelea kujizuia mpaka atakapochinja katika siku yoyote miongoni mwa siku za kubanika nyama.
Attribution
[Imepokelewa Imamu Muslim]
Categories
Share
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

