Atakayesema: (Laa ilaaha illa llahu, wah-dahu laa sharika lahu, Lahul mulku, Walahul hamdu, Wahuwa alaa kulli shaini Qadiir) kwa siku mara mia moja
Choose an available translation of this Hadeeth
Hadeeth text
Imepokelewa kutoka kwa Abuu Huraira -radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- yakwamba Mtume -rehema na amani ziwe juu yake- amesema: "Atakayesema: (Laa ilaaha illa llahu, wah-dahu laa sharika lahu, Lahul mulku, Walahul hamdu, Wahuwa alaa kulli shaini Qadiir) kwa siku mara mia moja, inakuwa kwakwe ni sawa na kuacha huru watu kumi, na anaandikiwa mema mia moja, na anafutiwa makosa mia moja, na inakuwa kwake ni kinga kutokana na Shetani kwa siku yake nzima mpaka afike jioni, na hatokuja yeyote na jambo bora zaidi kuliko atakalokuja nalo, isipokuwa yeyote atakayefanya zaidi ya alivyofanya yeye".
Explanation
Benefits
Upana wa fadhila za Mwenyezi Mungu Mtukufu juu ya waja wake, kiasi ambacho kawawekea dhikiri nyepesi kwa kila mmoja, na akaipangia thawabu nyingi.
Ikiwa atasema dhikiri hii (Tahalil) zaidi ya mara mia moja katika siku, basi atapata malipo yaliyotajwa katika hadithi ya mia moja, na atakuwa na thawabu nyingine za ziada, na hii si katika mipaka iliyozuiliwa kuivuka, na kupitiliza idadi yake, na kwamba kuzidisha kwake hakuna fadhila au kunaibatilisha.
Amesema Nawawi: Dhahiri ya ujumla wa hadithi hii nikuwa anayapata malipo haya yaliyotajwa katika hadithi ni yule atakayesema tahlil hii (dhikiri) mara mia moja katika siku yake, sawa sawa awe aliyasema kwa mfululizo au tofauti tofauti katika vikao tofauti, au baadhi yake mwanzo wa mchana na mengine mwisho wake, lakini kilicho bora ayalete mfululizo mwanzo wa mchana, ili iwe ni kinga kwake katika mchana wake wote.
Attribution
Categories
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

