Lau wangejua watu waliyomo katika Adhana na safu ya kwanza, kisha wasipate nafasi ila kwa kupiga kura ili kuyafikia basi wangelipiga kura
Choose an available translation of this Hadeeth
Hadeeth text
Kutoka kwa Abuu Huraira radhi za Allah ziwe juu yake yakwamba Mtume rehema na amani ziwe juu yake amesema: "Lau wangejua watu waliyomo katika Adhana na safu ya kwanza, kisha wasipate nafasi ila kwa kupiga kura ili kuyafikia basi wangelipiga kura, na walau wangelijua yaliyomo katika kuwahi basi wangelishindana, na lau wangelijua yaliyomo katika swala ya usiku na swala ya Asubuhi, basi wangeliziendea hata kwa kutambaa".
Explanation
Benefits
Kumebainishwa fadhila ya safu ya kwanza, na kuwa karibu na imamu.
Kumebanisha ubora wa kuwahi katika swala mwanzo wa wakati wake unaofaa; kwakuwa ndani yake kuna fadhila kubwa, na faida zinazoambatana na hilo, ikiwemo: Kuipata safu ya kwanza, na kuipata swala kuanzia mwanzo wake, na kutekeleza swala za sunna, na kusoma Qur'ani, na kupata kuombewa msamaha na Malaika, na kwamba anapata malipo kana kwamba yupo ndani ya swala kwa muda wote atakaokaa akisubiri swala, na mengineyo.
Himizo kubwa la kuhudhuria jamaa za swala hizi mbili, na fadhila nyingi katika hilo, kwa kuwa ndani yake kuna ugumu juu ya nafsi kama kuibana mwanzo wa usingizi wake na mwisho wake, na ndiyo maana zikawa ndio swala ngumu zaidi kwa wanafiki.
Amesema Nawawi: Hapa kuna kuthibitishwa kupiga kura katika haki ambazo watu wanasongamana na kuzozana ndani yake.
Safu ya pili ni bora kuliko safu ya tatu, na ya tatu ni bora kuliko ya nne, na kuendelea.
Attribution
Categories
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

