Hakika mja anaweza kuswali swala, hakuna anachoandikiwa isipokuwa moja ya kumi yake, moja ya tisa yake, nane ya kumi yake, saba ya kumi yake, sita ya kumi yake, tano ya kumi yake, robo yake, theluthi yake, nusu yake
Choose an available translation of this Hadeeth
Hadeeth text
Kutoka kwa Abdallah bin Anama, amesema: Nilimuona Ammari bin Yasiri aliingia Msikitini akaswali, akaifanya swala kuwa fupi, akasema: Alipotoka, Nilisimama kwa ajili ya kumfuata, kisha nikasema: Ewe baba Yakdhani, umefupisha sana, akasema: Je, umeniona nimepunguza chochote katika mipaka yake?! Nikasema: Hapana, akasema: Hakika mimi nilikwenda mbio ili kukwepa kusahaulishwa na Shetani, nilimsikia Mtume rehema na amani ziwe juu yake akisema: "Hakika mja anaweza kuswali swala, hakuna anachoandikiwa isipokuwa moja ya kumi yake, moja ya tisa yake, nane ya kumi yake, saba ya kumi yake, sita ya kumi yake, tano ya kumi yake, robo yake, theluthi yake, nusu yake".
Explanation
Benefits
Kupata uhakika na kuuliza kabla ya kukemea.
Inatosha kujibu swali na utata kwa kauli ya Mtume rehema na amani ziwe juu yake.
Kupungua kwa malipo ya swala kwa kupungua kwa utulivu na mazingatio ndani yake.
Himizo kubwa na msisitizo mkubwa juu ya kuwa na utulivu ndani ya swala na moyo kuhudhuria na kuwa pamoja na Mwenyezi Mungu.
Attribution
Categories
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

