HadeethEnc · 1.18.0
Yakuwa aliulizwa kuhusu kisomo cha Mtume rehema na amani ziwe juu yake
Available translations
Choose an available translation of this Hadeeth
01
Hadeeth text
Kutoka kwa Abuu Mulaika: Kutoka kwa baadhi ya wake za Mtume rehema na amani ziwe juu yake, amesema: Abuu Aamir, amesema Naafii: Nafikiri ni Hafswa -Yakuwa aliulizwa kuhusu kisomo cha Mtume rehema na amani ziwe juu yake akasema: Hakika nyinyi hamkiwezi, akasema: Akaambiwa hebu tueleze. Akasema: Akasoma kisomo cha taratibu, akasema Abuu Aamiri: Akasema Naafii: Akatusimulia Abuu Mulaika: "Alhamdulillaah Rabbil-Aalamiin" [Al-Faatiha: 1] Kisha akakata "Al Rahmaanir Rahiim" [Faatiha:3] kisha akakata "Maaliki yaumid diin".
02
Explanation
Aliulizwa Hafswa mama wa waumini radhi za Allah ziwe juu yake: Kilikuwa vipi kisomo cha Qur'ani cha Mtume rehema na amani ziwe juu yake? Akasema: Hakika nyinyi hamkiwezi mfano wake, akaambiwa: Tueleze. Amesema Naafii: Akatusomea Abuu Mulaika kisomo alichotulizana ndani yake; ili kielezee na kikaribiane na kisomo cha Mtume rehema na amani ziwe juu yake, akasoma: "Alhamdulillaahi Rabbil Aalamiin" kisha akakata kisomo, "Al Rahmaanir Rahiim", kisha akakata kisomo, "Maaliki yaumid diin".
03
Benefits
Kumebainishwa muongozo wa Mtume rehema na amani ziwe juu yake katika kusoma Qur'ani.
Kufanya kwa vitendo ili kubainisha namna ya kisomo cha Mtume rehema na amani ziwe juu yake.
Sheria ya kwenda taratibu katika kuisoma Qur'ani, hilo huleta msukumo wa kuizingatia.
Kuitilia maanani Qur'ani wema waliotangulia, na matendo ya Mtume rehema na amani ziwe juu yake.
Umuhimu wa kujua kanuni za kuisoma Qur'ani (Tajwidi) na elimu za Qur'ani.
Kufanya kwa vitendo ili kubainisha namna ya kisomo cha Mtume rehema na amani ziwe juu yake.
Sheria ya kwenda taratibu katika kuisoma Qur'ani, hilo huleta msukumo wa kuizingatia.
Kuitilia maanani Qur'ani wema waliotangulia, na matendo ya Mtume rehema na amani ziwe juu yake.
Umuhimu wa kujua kanuni za kuisoma Qur'ani (Tajwidi) na elimu za Qur'ani.
Attribution
[Imepokelewa na Ahmad]
Categories
Share
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

