Imani ni zaidi ya vitengo sabini au zaidi ya sitini, bora yake ni kauli ya Laa ilaaha illa llaah, na ya chini yake ni kuondoa udhia barabarani
Choose an available translation of this Hadeeth
Hadeeth text
Imepolelewa Kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Allah ziwe juu yake- amesema: amesema: Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake-: "Imani ni zaidi ya vitengo sabini au zaidi ya sitini, bora yake ni kauli ya Laa ilaaha illa llaah, na ya chini yake ni kuondoa udhia barabarani, na haya ni sehemu katika imani".
Explanation
Nakuwa jambo la juu zaidi katika mambo ya imani ni kauli ya: Laa ilaaha illa llaah", kwa kujua maana yake, na kufanyia kazi matakwa yake, yakuwa Mwenyezi Mungu ndiye Mola Mlezi Mmoja wa pekee mwenye kustahaki kuabudiwa peke yake pasina mwingine zaidi yake.
Nakuwa tendo dogo kabisa katika matendo ya imani ni kila chenye kuwaudhi watu katika njia zao.
Kisha akaeleza -Rehema na amani ziwe juu yake- kuwa haya ni katika mambo ya imani, nayo ni tabia inayomsukuma mtu kufanya mazuri na kuacha mabaya.
Benefits
Imani ni kauli na matendo na itikadi.
Kumuonea haya Allah Mtukufu hupelekea: Kuwa asikuone pale alipokukataza, na asikukose pale alipokuamrisha.
Kutajwa idadi hakumaanishi kuishia hapo, bali inamaanisha wingi wa matendo ya imani, kwani waarabu wanaweza kutaja idadi ya kitu na wasimaanishe kukanusha idadi nyingine isiyokuwa hiyo.
Attribution
Categories
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

