HadeethEnc · 1.18.0
Atakayemuua aliyechukua ahadi ya kulindwa, hatonusa harufu ya pepo, na hakika hurufu yake hupatikana kuanzia mwendo wa miaka arobaini
Available translations
Choose an available translation of this Hadeeth
01
Hadeeth text
Imepokewa Kutoka kwa Abdillah Ibn Amri -Radhi za Allah ziwe juu yao wawili- kutoka kwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake-amesema: "Atakayemuua aliyechukua ahadi ya kulindwa, hatonusa harufu ya pepo, na hakika hurufu yake hupatikana kuanzia mwendo wa miaka arobaini".
02
Explanation
Anabainisha Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- tahadhari kubwa kwa atakayemuuwa aliyechukua ahadi ya kulindwa -Naye ni kafiri aliyeingia katika mji wa kiislamu kwa ahadi na amani- kuwa hatonusa harufu ya Pepo, na hakika harufu yake huwa kuanzia umbali wa mwendo wa miaka arobaini.
03
Benefits
Uharamu wa kumuua aliyechukua ahadi ya amani na kafiri anayeishi na waislamu, na aliyeomba amani katika makafiri, nakuwa jambo hilo ni dhambi kubwa katika madhambi makubwa.
Aliyechukua ahadi: Ni kafiri aliyechukua ahadi ya kutowapiga vita waislamu na huku akiishi katika mji wake, na wao wasimpige vita, na dhimi: Ni yule anayeishi mji wa waislamu na akalipa jizia (kodi ya kichwa), na muomba amani: Ni mtu aliyeingia mji wa waislamu kwa mkataba na amani kwa muda maalumu.
Tahadhari ya kufanya hiyana katika makubaliano na wasiokuwa waislamu.
Aliyechukua ahadi: Ni kafiri aliyechukua ahadi ya kutowapiga vita waislamu na huku akiishi katika mji wake, na wao wasimpige vita, na dhimi: Ni yule anayeishi mji wa waislamu na akalipa jizia (kodi ya kichwa), na muomba amani: Ni mtu aliyeingia mji wa waislamu kwa mkataba na amani kwa muda maalumu.
Tahadhari ya kufanya hiyana katika makubaliano na wasiokuwa waislamu.
Attribution
[Imepokelewa na Al-Bukhaariy]
Categories
Share
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

