HadeethEnc · 1.18.0
Alikuwa Mtume wa Allah -rehema na amani ziwe juu yake ni mkarimu kuliko watu wote, na alikuwa mkarimu zaidi anapokuwa katika mwezi wa Ramadhani pindi anapokutana na Jibrili
Available translations
Choose an available translation of this Hadeeth
01
Hadeeth text
Imepokelewa kutoka kwa bin Abbas -radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- amesema: Alikuwa Mtume wa Allah -rehema na amani ziwe juu yake ni mkarimu kuliko watu wote, na alikuwa mkarimu zaidi anapokuwa katika mwezi wa Ramadhani pindi anapokutana na Jibrili, na alikuwa akikutana naye katika kila usiku wa Ramadhani akimsomesha Qur'ani, basi hakika Mtume wa Mwenyezi Mungu -rehema na Amani ziwe juu yake- ni mkarimu zaidi kwa mambo ya kheri kuliko hata upepo uliotumwa.
02
Explanation
Mtume rehema na amani ziwe juu yake alikuwa mkarimu zaidi kuliko watu wote katika mwezi wa Ramadhani, kiasi ambacho alikuwa akitoa kinachostahiki kumpa anayestahiki, na sababu ya kuzidisha ukarimu huu ni mambo mawili:
La kwanza: Ni kukutana kwake na Jibril amani iwe juu yake.
Na jambo jingine: Ni kuirejea Qur'ani, nayo ni kuisoma pasina kutazama mahali ilipoandikwa.
Kwa hiyo Jibril, amani iwe juu yake, alisoma naye kila kilichoteremshwa katika Qur'ani, na Mtume wa Mwenyezi Mungu rehema na amani ziwe juu yake ni mkarimu zaidi, na ni mtenda kheri zaidi, na ni mwepesi wa kunufaisha viumbe kuliko upepo mzuri anaoutuma Mwenyezi Mungu kwa ajili ya mvua na rehema.
La kwanza: Ni kukutana kwake na Jibril amani iwe juu yake.
Na jambo jingine: Ni kuirejea Qur'ani, nayo ni kuisoma pasina kutazama mahali ilipoandikwa.
Kwa hiyo Jibril, amani iwe juu yake, alisoma naye kila kilichoteremshwa katika Qur'ani, na Mtume wa Mwenyezi Mungu rehema na amani ziwe juu yake ni mkarimu zaidi, na ni mtenda kheri zaidi, na ni mwepesi wa kunufaisha viumbe kuliko upepo mzuri anaoutuma Mwenyezi Mungu kwa ajili ya mvua na rehema.
03
Benefits
Kumebainishwa ukarimu wa Mtume rehema na amani ziwe juu yake na upana wa ukarimu wake hasa katika mwezi wa Ramadhani, kwani ni mwezi wa utiifu na misimu ya matendo mema.
Himizo la ukarimu kila wakati, na ni sunna kuzidisha zaidi katika mwezi wa Ramadhani.
Kukithirisha utoaji wa misaada na ihsani na kusoma Qur'ani katika mwezi wa Ramadhani.
Katika sababu za kuihifadhi elimu ni kujisomea pamoja na wanafunzi wengine na wanachuoni.
Himizo la ukarimu kila wakati, na ni sunna kuzidisha zaidi katika mwezi wa Ramadhani.
Kukithirisha utoaji wa misaada na ihsani na kusoma Qur'ani katika mwezi wa Ramadhani.
Katika sababu za kuihifadhi elimu ni kujisomea pamoja na wanafunzi wengine na wanachuoni.
Attribution
[Wamekubaliana Bukhari na Muslim juu ya usahihi wake]
Categories
Share
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

