Je, nisikujulisheni kitu bora zaidi kuliko hicho mlichoomba? Mtakapokwenda kulala basi msabihini Mwenyezi Mungu; yaani (Sub-haanallaah) mara thelathini na tatu, na mhimidini (Al-hamdulillaah) mara thelathini na tatu, na mtukuzeni (Allahu Akbar) mara thelathini na nne, kufanya hivyo ni bora zaidi kwenu kuliko mfanyakazi.”
Choose an available translation of this Hadeeth
Hadeeth text
Imepokelewa kutoka kwa Ally -radhi za Allah ziwe juu yake-: ِAlikuja Fatma radhi za Allah ziwe juu yake kwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake akimlalamikia juu ya jiwe la kusagia lililokuwa likichubua mikono yake, na zilimfikia taarifa kuwa Mtume amejiwa na mjakazi, lakini alikuwa hajakutana naye, akalieleza hilo kwa Aisha, alipokuja Aisha akamwambia, anasema Fatma: Akaja kwetu hali yakuwa tumekwisha panda kitandani, basi tukaamka tukasimama, akasema: "Haina haja ya kusimama kaeni tu mahala penu" Akaja akakaa kati yangu na Fatma, mpaka nikahisi ubaridi wa miguu yake tumboni kwangu, Mtume akasema: «Je, nisikujulisheni kitu bora zaidi kuliko hicho mlichoomba? Mtakapokwenda kulala basi msabihini Mwenyezi Mungu; yaani (Sub-haanallaah) mara thelathini na tatu, na mhimidini (Al-hamdulillaah) mara thelathini na tatu, na mtukuzeni (Allahu Akbar) mara thelathini na nne, kufanya hivyo ni bora zaidi kwenu kuliko mfanyakazi.”
Explanation
Benefits
Dhikiri hii haisemwi tu wakati wa kulala usiku, na maneno yake kwa mujibu wa Muslim yanatokana na riwaya ya Muadhi kutoka kwa Shu’ba: “Mkichukua vitanda vyenu wakati wa usiku.”
Muislamu akiisahau dhikri hii mwanzoni mwa usiku kisha akaikumbuka mwishoni mwa usiku, hakuna ubaya kuisema; Kwa sababu Ally Mwenyezi Mungu amuwie radhi, msimuliaji wa hadithi, anasema kwamba alisahau kuyasema katika usiku wa mapigano ya Swaffin mwanzoni mwa usiku, kisha akakumbuka na kuyasema kabla ya Alfajiri.
Amesema Al-Muhallab: Ndani ya Hadithi hii kunaonyesha kuwa mtu ailazimishe familia yake kufanya anayojilazimisha yeye, kama kutanguliza maisha ya Akhera kuliko Dunia hii ikiwa wana uwezo wa kufanya hivyo.
Amesema bin Hajar Al-Asqalani: Atakayedumu na dhikiri hii hatadhurika na wingi wa kazi, wala haitakuwa vigumu kwake hata akichoka.
Amesema Al-Aini: Suala la kuwa bora ni ima maana yake ni kuwa inahusiana na Akhera na mfanyakazi duniani, na Akhera ni bora zaidi na yenye kudumu, au ina maana kwamba kuhusiana na kile alichoomba atapata nguvu kwa sababu ya dhikiri hii ambayo itamuwezesha kufanya kazi zaidi kuliko uwezo wa mfanyakazi.
Attribution
Categories
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

