HadeethEnc · 1.18.0
Sharti zenye haki zaidi kwenu nyinyi kuzitekeleza ni zile mlizohalalishia tupu
Available translations
Choose an available translation of this Hadeeth
01
Hadeeth text
Imepokewa kutoka kwa Uqbah Bin Aamir -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake-amesema: Amesema Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake: "Sharti zenye haki zaidi kwenu nyinyi kuzitekeleza ni zile mlizohalalishia tupu".
02
Explanation
Anabainisha Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- yakuwa sharti bora kabisa kwa kutekelezwa ni zile zilizokuwa sababu ya uhalali wa kustarehe na mwanamke, nazo ni zile sharti za halali anazozitaka mwanamke wakati wa kufunga ndoa.
03
Benefits
Uwajibu wa kutekeleza sharti ambazo amezitilia umuhimu mmoja kati ya wanandoa wawili kwa mwenzie, isipokuwa sharti itakayoharamisha halali au kuhalalisha haramu.
Kutekeleza sharti za ndoa kumetiliwa mkazo kuliko sharti zote; kwa sababu huambatana na kuhalalisha tupu.
Ukubwa wa nafasi ya ndoa katika Uislamu, kiasi ambacho umetilia mkazo juu ya kutimiza sharti zake.
Kutekeleza sharti za ndoa kumetiliwa mkazo kuliko sharti zote; kwa sababu huambatana na kuhalalisha tupu.
Ukubwa wa nafasi ya ndoa katika Uislamu, kiasi ambacho umetilia mkazo juu ya kutimiza sharti zake.
Attribution
[Wamekubaliana Bukhari na Muslim juu ya usahihi wake]
Categories
Share
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

