Namuapa yule ambaye nafsi yangu iko mkononi mwake mtafuata nyenendo za wale waliokuwa kabla yenu
Choose an available translation of this Hadeeth
Hadeeth text
Kutoka kwa Abuu Waaqidi All-laithi radhi za Allah ziwe juu yake. Yakuwa Mtume rehema na amani zimfikie alipotoka kwenda katika vita vya Hunaini alipita katika mti wa washirikina ukiitwa: Dhata anwatwi (Mahala pa kutundika silaha) wakitundika silaha zao hapo, wakasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, tuwekee nasi mahala pa kutundikia kama ambavyo wao wana mahala pa kutundikia, akasema Mtume rehema na amani zimfikie: "Sub-haanallaah (Ametakasika Mwenyezi Mungu)! Maneno haya ni kama yale waliyosema watu wa Mussa: "Tufanyie nasi mungu kama walivyo wao na mungu" [Al-A'raaf: 138] Namuapa yule ambaye nafsi yangu iko mkononi mwake mtafuata nyenendo za wale waliokuwa kabla yenu".
Explanation
Benefits
Ni wajibu kwa Muislamu kumtukuza Mwenyezi Mungu (Kumsabihi) na kutoa takbira anaposikia maneno yasiyofaa kusemwa katika dini, na wakati wa kustaajabu.
Ni katika shirki kutaka baraka katika miti na mawe na vinginevyo, na baraka hazitafutwi ila kutoka kwa Mwenyezi Mungu peke yake.
Sababu za kuabudu masanam ni kuyatukuza, na kukaa hapo, na kuyataka baraka.
Uwajibu wa kuziba milango na njia zinazopelekea katika ushirikina.
Dalili zilizokuja kuwasema kwa ubaya Mayahudi na Wakristo ni tahadhari kwetu.
Katazo la kujifananisha na watu wajinga na Mayahudi na Wakristo, isipokuwa katika yale ambayo dalili zimekuja kuwa ni katika dini yetu.
Attribution
Categories
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

