Amewalaani Mwenyezi Mungu Mayahudi na Wakristo, waliyafanya makaburi ya Manabii wao kuwa mahali pa kusalia
Choose an available translation of this Hadeeth
Hadeeth text
Kutoka kwa Aisha mama wa waumini radhi za Allah ziwe juu yake amesema: Amesema Mtume rehema na amani ziwe juu yake akiwa katika maradhi yake ambayo hakuweza kuamka tena: "Amewalaani Mwenyezi Mungu Mayahudi na Wakristo, waliyafanya makaburi ya Manabii wao kuwa mahali pa kusalia" Akasema: Na lau kama isingekuwa kauli hiyo basi lingenyanyuliwa kaburi lake, isipokuwa ilihofiwa kufanywa kuwa mahali pa kuswalia.
Explanation
Benefits
Katazo la msisitizo na uharamu mkubwa wa kuyafanya makaburi kuwa mahali pa kuswalia, na kuyaendea kwa ajili ya kuswali hapo swala isiyokuwa swala ya jeneza; huu ni upenyo wa kumtukuza maiti na kutufu (kuzunguka) katika kaburi lake, na kujifuta kwa nguzo zake (za kaburi), na kumuita kwa jina lake, na yote hayo ni katika ushirikina na ni katika njia zake.
Ukubwa wa kutilia umuhimu na kutilia maanani Mtume rehema na amani ziwe juu yake Tauhidi, na hofu yake juu ya kutukuzwa makaburi; kwa sababu hilo linapelekea katika ushirikina.
Mwenyezi Mungu Mtukufu alimlinda Nabii wake amani iwe juu yake, isijekufanywa shirki juu ya kaburi lake, akawapa maono Maswahaba wake na wale wanaokuja baada yao, walilinde kaburi lake lisije kunyanyuliwa.
Maswahaba kuufanyia kazi usia wa Mtume rehema na amani ziwe juu yake na pupa yao juu ya Tauhidi.
Katazo la kujifananisha na Mayahudi na Wakristo, na kwamba kuyajengea makaburi ni katika tamaduni zao.
Miongoni mwa aina za kuyafanya makaburi kuwa misikiti ni kuswali hapo, hata kusipojengwa msikiti.
Attribution
Categories
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

