Wasikilizeni na muwatii, kwani wao wana yao waliyobebeshwa nanyi mna yenu mliyobebeshwa
Choose an available translation of this Hadeeth
Hadeeth text
Kutoka kwa Wail bin Hadhrami amesema: Salama bin Yazidi Al-Ju'fi radhi za Allah ziwe juu yake alimuuliza Mtume rehema na amani ziwe juu yake, akasema: Ewe Nabii wa Mwenyezi Mungu, hebu tueleze endapo watasimama viongozi wetu wakituomba haki zao, na hali wao wanazuia haki zetu, unatuamrisha nini? Mtume akampuuza, kisha akamuuliza, akampuuza, kisha akamuuliza katika mara ya pili au ya tatu, Ash'athi bin Kaisi akamvuta, na akasema: "Wasikilizeni na muwatii, kwani wao wana yao waliyobebeshwa nanyi mna yenu mliyobebeshwa"
Explanation
Mtume rehema na amani ziwe juu yake akampuuza; kana kwamba kalichukia swali hili, lakini muulizaji akarudia mara ya pili na ya tatu, Ash'athi bin Kaisi akamvuta muulizaji ili amnyamazishe.
Mtume rehema na amani ziwe juu yake akajibu na akasema: Sikilizeni kauli zao, na mtii amri zao; kwani wana yao waliyobebeshwa na kulazimishwa kuyafanya ikiwemo uadilifu na raia kuwapa haki zao, na nyinyi mna yenu mliyobebeshwa kama kutii na kutimiza haki na kusubiri juu ya mabalaa.
Benefits
Uzembe wa viongozi katika kutimiza wajibu wao, haupelekei watu wengine kufanya uzembe ili kulipiza kisasi katika wajibu wao; kila mmoja ataulizwa juu ya matendo yake, na atahukumiwa kwa uzembe wake.
Dini haijajengwa katika misingi ya nipe nikupe, bali katika misingi ya kushikamana na yale ya wajibu hata kama mtu mwingine hatotenda haki kwa yale ya wajibu kwake kwa wakati huo, kama ilivyokuja katika hadithi hii.
Attribution
Categories
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

