Kila kiungo kwa watu kina sadaka
Choose an available translation of this Hadeeth
Hadeeth text
Imepokelewa kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Allah ziwe juu yake- amesema: Amesema Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake-: "Kila kiungo kwa watu kina sadaka, kila siku inayochomozewa jua: Ukafanya uadilifu kati ya watu wawili ni sadaka, na ukimsaidia mtu katika mnyama wake ukambeba kumpandisha au ukamnyanyulia mzigo wake ni sadaka, na neno zuri ni sadaka, na kwa kila hatua unayokwenda kuelekea msikitini ni sadaka, na ukiondoa maudhi njiani ni sadaka".
Explanation
Benefits
Himizo la kurudia upya shukurani kila siku ili neema hizo zidumu.
Himizo la kudumu kufanya ibada za sunna na sadaka kila siku.
Fadhila ya kusuluhisha baina ya watu.
Himizo la mtu kumsaidia ndugu yake; kwani msaada wake kwake ni sadaka.
Himizo la kuhudhuria swala za pamoja na kuziendea, na kuimarisha misikiti kwa hilo.
Uwajibu wa kuheshimu njia wanazopita waumini kwa kuepuka yanayo waudhi au kuwadhuru.
Attribution
Categories
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

