Mfano wa yule anayemtaja Mola wake na yule asiyemtaja Mola wake, ni mfano wa aliyehai na aliyekufa
Choose an available translation of this Hadeeth
Hadeeth text
Na kutoka kwa Abuu Musa -radhi za Allah ziwe juu yake- amesema: Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu -rehema na amani ziwe juu yake: "Mfano wa yule anayemtaja Mola wake na yule asiyemtaja Mola wake, ni mfano wa aliyehai na aliyekufa", Na tamko la Muslim: "Mfano wa nyumba anayotajwa Mwenyezi Mungu ndani yake, na nyumba asiyotajwa Mwenyezi Mungu ndani yake, ni mfano wa aliyehai na aliyekufa".
Explanation
Na vile vile nyumba inasifiwa kwa sifa ya kuwa hai endapo wakazi wake wanamtaja Mwenyezi Mungu, na vinginevyo itakuwa nyumba mfu kwa kubweteka wakazi wake na kutomtaja Mwenyezi Mungu; na nyumba ikiitwa hai na maiti wanakusudiwa wakazi wa nyumba hiyo.
Benefits
Dhikri ndio uhai wa roho kama ambavyo roho ni uhai wa mwili.
Katika muongozo wa Mtume rehema na amani ziwe juu yake ni kupiga mifano ili kusogeza karibu maana.
Amesema Imam Nawawi: Hapa kuna wito wa kuja katika kumtaja Mwenyezi Mungu Mtukufu ndani ya nyumba, nakuwa haiachwi tupu pasina kumtaja Mwenyezi Mungu.
Amesema Nawawi: Na pia kuwa na umri mrefu katika utiifu ni fadhila hata ikiwa maiti atahama kwenda katika kheri zaidi; kwa sababu aliyehai anampata na kumzidi kwa yale anayoyafanya katika mambo ya kumtii Mwenyezi Mungu.
Attribution
Categories
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

