HadeethEnc · 1.18.0
Yakwamba mtu mmoja alimuuliza Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- na mguu wake ukiwa tayari umeuweka kwenye kipandwa (yaani yuko tayari kwa safari): Ni jihadi ipi bora? Akasema: ni neno la haki kwa kiongozi muovu
Available translations
Choose an available translation of this Hadeeth
01
Hadeeth text
Kutoka kwa Twariq bin Shihabi Al bajaliy Al Ahmashiy -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Yakwamba mtu mmoja alimuuliza Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- na mguu wake ukiwa tayari umeuweka kwenye kipandwa (yaani yuko tayari kwa safari): Ni jihadi ipi bora? Akasema: "Ni neno la haki kwa kiongozi muovu".
02
Explanation
Mtu mmoja alimuuliza Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake akiwa tayari kajiandaa kwaajili ya safari: Ni jihadi ipi yenye thawabu nyingi? Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- akamueleza kuwa jihadi bora, ni yeye kumuamrisha mema kiongozi dhalimu, au amkataze maovu, jihadi haishii pekee kupigana na makafiri, bali ina daraja, na iliyotajwa ndiyo ina malipo mengi zaidi; kwasababu inahofiwa mtu kuuawa au kukamatwa kwasababu ya ujeuri na kiburi cha kiongozi na kwasababu ya uchache wa wenye kujitosa katika hilo.
Attribution
[Imepokelewa na An-Nasaaiy - Imepokelewa na Ahmad]
Categories
Share
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

