HadeethEnc · 1.18.0
Hakuwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuwa na mkazo mkubwa na kudumu na jambo kama alivyokuwa katika rakaa mbili za Alfajiri
Available translations
Choose an available translation of this Hadeeth
01
Hadeeth text
Imepokelewa kutoka kwa Aisha mama wa waumini radhi za Allah ziwe juu yake, amesema: Hakuwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuwa na mkazo mkubwa na kudumu na jambo kama alivyokuwa katika rakaa mbili za Alfajiri.
02
Explanation
Ameeleza mama wa waumini Aisha radhi za Allah ziwe juu yake ya kwamba Mtume rehema na amani ziwe juu yake hakuwa na mkazo mkubwa katika swala za sunna zaidi ya jinsi alivyozikazia na kuzipupia na kuzihifadhi rakaa mbili za sunna ya kabla ya Alfajiri.
03
Benefits
Sunna za swala ni zile zisizokuwa faradhi katika ibada, na makusudio yake hapa: Ni sunna zilizopangilia zinazofuatana na faradhi.
Sunna zilizopangiliwa: Rakaa mbili kabla ya Alfajiri, na rakaa nne kabla ya Adhuhuri, na mbili baada yake, na rakaa mbili baada ya Magharibi, na rakaa mbili baada ya Ishaa.
Sunna ya Alfajiri huswaliwa nyumbani na safarini, tofauti na sunna za Adhuhuri na Magharibi na Ishaa, hizo haziswaliwi isipokuwa nyumbani.
Sunna hii imetikiliwa mkazo ya rakaa mbili za Alfajiri, haitakiwi kuzipuuza.
Sunna zilizopangiliwa: Rakaa mbili kabla ya Alfajiri, na rakaa nne kabla ya Adhuhuri, na mbili baada yake, na rakaa mbili baada ya Magharibi, na rakaa mbili baada ya Ishaa.
Sunna ya Alfajiri huswaliwa nyumbani na safarini, tofauti na sunna za Adhuhuri na Magharibi na Ishaa, hizo haziswaliwi isipokuwa nyumbani.
Sunna hii imetikiliwa mkazo ya rakaa mbili za Alfajiri, haitakiwi kuzipuuza.
Attribution
[Wamekubaliana Bukhari na Muslim juu ya usahihi wake]
Categories
Share
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

