Mtu atakayepata furaha zaidi ya uombezi wangu siku ya Kiyama, ni yule atakayesema Laa ilaaha illa llah (Hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu), kwa kutakasa nia toka moyo mwake au nafsi yake
Choose an available translation of this Hadeeth
Hadeeth text
Imepokelewa Kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Allah ziwe juu yake- amesema: Palisemwa ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu ni mtu gani atakayepata furaha zaidi ya uombezi wako siku ya Kiyama? Akasema Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake-: "Nilijua kuwa ewe Abuu Huraira hatoniuliza mwingine hadithi hii kabla yako, kwa kile nilichokiona kwako, pupa yako juu ya hadithi, Mtu atakayepata furaha zaidi ya uombezi wangu siku ya Kiyama, ni yule atakayesema Laa ilaaha illa llah (Hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu), kwa kutakasa nia toka moyo mwake au nafsi yake".
Explanation
Benefits
Uombezi wake -Rehema na amani ziwe juu yake- ni kuomba kwake kupitia kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa yule atakaye stahiki Moto katika watu wa tauhidi ili asiuingie, na aliyeuingia atoke.
Ubora wa neno la tauhidi lililotakasiwa nia kwa ajili ya Allah Mtukufu na athari zake kubwa.
Kulihakikisha neno la tauhidi kunakuwa kwa kujua maana yake, na kufanyia kazi makusudio yake kwa namna inavyotakikana.
Ubora wa Abuu Huraira -Radhi za Allah ziwe juu yake-, na pupa yake juu ya elimu.
Attribution
Categories
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

