HadeethEnc · 1.18.0
Sikumuona Mtume -rehema amani ziwe juu yake- katu akipitiliza kucheka mpaka kionekane Kilimi ndani ya mdomo wake, bali alikuwa akitabasamu
Available translations
Choose an available translation of this Hadeeth
01
Hadeeth text
Imepokelewa kutoka kwa Aisha mama wa waumini radhi za Allah ziwe juu yake, amesema: Sikumuona Mtume -rehema amani ziwe juu yake- katu akipitiliza kucheka mpaka kionekane Kilimi ndani ya mdomo wake, bali alikuwa akitabasamu.
02
Explanation
Alieleza Aisha radhi za Allah ziwe juu yake kuwa Mtume rehema amani ziwe juu yake alikuwa hapitilizi kucheka mpaka kionekane kilimi chake, nacho ni kinyama kinachoning'inia juu ya koo, bali alikuwa akitabasam.
03
Benefits
Kulikuwa kucheka kwa Mtume rehema amani ziwe juu yake ni kutabasam anaporidhia au kufurahishwa na jambo.
Amesema bin Hajari: Sikuwahi kumuona akipitiliza katika kucheka kiasi cha kucheka kicheko kamili kwa kujiachia mzima mzima kwa kicheko.
Kukithirisha kucheka na kunyanyua sauti kwa kujikohoza hii si miongoni mwa sifa za watu wema.
Kukithirisha kucheka kunaondoa haiba ya mtu na heshima yake mbele ya ndugu zake.
Amesema bin Hajari: Sikuwahi kumuona akipitiliza katika kucheka kiasi cha kucheka kicheko kamili kwa kujiachia mzima mzima kwa kicheko.
Kukithirisha kucheka na kunyanyua sauti kwa kujikohoza hii si miongoni mwa sifa za watu wema.
Kukithirisha kucheka kunaondoa haiba ya mtu na heshima yake mbele ya ndugu zake.
Attribution
[Wamekubaliana Bukhari na Muslim juu ya usahihi wake]
Categories
Share
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

