Anayesoma Qur'ani kwa uhodari huwa pamoja na msafara wa Malaika watukufu, na anayesoma Qur'ani huku anasitasita na huku kwake bado ni ngumu huyo anamalipo mara mbili
Choose an available translation of this Hadeeth
Hadeeth text
Kutoka kwa Aisha radhi za Allah ziwe juu yake amesema: Amesema Mtume rehema na amani ziwe juu yake: "Anayesoma Qur'ani kwa uhodari huwa pamoja na msafara wa Malaika watukufu, na anayesoma Qur'ani huku anasitasita na huku kwake bado ni ngumu huyo anamalipo mara mbili".
Explanation
Benefits
Amesema Kadhi: Na haina maana kuwa anayesitasita ana malipo makubwa zaidi kuliko mahiri, bali mahiri ndiye bora na ndiye mwenye malipo mengi; kwa sababu yuko pamoja na Malaika na anamalipo mengi, na hakutaja nafasi hii kwa mwingine, ni vipi ataungana naye ambaye hajakipa kipaumbele kitabu cha Mwenyezi Mungu Mtukufu na kukihifadhi na kuwa na umahiri na wingi wa kukisoma na kukielewa kwake ni kama kukipa kipaumbele mpaka akawa mahiri ndani yake.
Amesema bin Bazi: Anayesoma Qur'ani hali yakuwa ni mahiri, na anaisoma vizuri, na anaihifadhi vizuri yuko pamoja na Malaika wema watukufu, yaani: Ikiwa kama ataisoma kwa kauli na matendo, na si ilimradi kuisoma pekee, anaisoma vizuri, na anaifanyia kazi, yaani anaisimamia kwa lafudhi na maana.
Attribution
Categories
Share hadeeth
Sharing options · 0 Total shares

